Sunday, April 3, 2011

Best Blogger Tips
Wabunge 'mabubu' wanyooshewa kidole

Via Majira

UTAFITI uliofanywa juu ya utendaji kazi wa wabunge, katika bunge la tisa, umetoa tahadhari kwa wabunge wa bunge la 10 wasiochangia kukaa
mkao wa kutorudi bungeni, huku vyama vyao vikihadharishwa kuwa vitaadhibiwa kwa kuzidi kupoteza wawakilishi.

Tahadhari hiyo imetokana na utafiti huo kubaini kuwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana, moja ya vigezo ambavyo wapiga kura walivitumia ilikuwa ni kuzingatia kiwango cha ushiriki wa wabunge katika bunge la tisa.

Kutokana na kuzingatia kiwango hicho cha kushiriki katika kuchangia mijadala, chama kilichokuwa na ushiriki mdogo bungeni, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeonekana kuadhibiwa kwa kupoteza viti vingi, ambapo chama kilichokuwa na ushiriki mkubwa bungeni (CHADEMA) kimefanikiwa kuongeza viti.

"Kidokezo kinachojitokeza katika matokeo haya kwa bunge la 10 ni kwamba vyama vya siasa vyenye nia ya kukua katika siku zijazo vitahitaji kuwahimiza wabunge wao kuwa washiriki wazuri katika shughuli za bunge," imesema sehemu ya utafiti huo uliofanywa na asasi binafsi maarufu ya Uwazi, iliyoko chini ya Twaweza.

Asasi hiyo ambayo imeshafanya tafiti mbalimbali, zilizoibua mijadala mikubwa nchini, ikiwa ni changamoto kwa wahusika, kama ule wa wahitimu wa darasa la saba kutoweza kumudu masomo ya darasa la pili, imetumia tovuti ya bunge katika kukusanya takwimu za taarifa yake hiyo.
Endelea kusoma habari hii.......................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits