Tuesday, April 5, 2011

Best Blogger Tips
Mama wa Rais Kabila apata kikombe

Via mwananchi

SASA ni dhahiri kwamba tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Ambilikile Mwasapila, imesambaa na kuvuka mipaka ya nchi na kuanza kuzigusa familia za vigogo.Juzi, mama mzazi wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC), Joseph Kabila alifika katika Kijiji cha Samunge, Loliondo, Wilaya ya Ngorongoro na kupata kikombe cha dawa.

Mama huyo, Sifa Maanya Kabila aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Wasso, Loliondo majira ya mchana kwa siri na kwenda moja kwa moja katika Kijiji cha Samunge ambako alipata dawa pamoja na ujumbe wake wa watu wasiozidi saba, wengi wakiwa ni kina mama.

Mwananchi lilishuhudia Mama Sifa akipanda ndege katika Uwanja za Wasso juzi jioni pamoja na ujumbe wake wakiondoka huku wakisindikizwa na Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali na maofisa wa usalama.
 Hata hivyo, Lali alipohojiwa na Mwananchi kuhusu ujio wa Mama yake Rais Kabila alisema, hakuwa akiwafahamu waliokuwamo kwenye ndege hiyo na kudai kwamba alifika kumwombea msaada wa usafiri ndugu yakealiyekuwa akienda mjini Arusha.

Lakini, chanzo chetu cha habari kilithibitisha pasi na shaka kwamba ndege hiyo ilikuwa na ujumbe wa mama mzazi wa Rais Kabila. "Ni watu kutoka Kongo (DRC) na wameambatana na mama mzito kidogo ambaye ni mama mzazi wa Rais Kabila, wengine nadhani ni watu waliomsindikiza tu," kilisema chanzo chetu cha habari kilichokuwa katika msafara huo.Ujumbe wa Mama Sifa Kabila ulipanda ndege hiyo ya kukodi kuelekea mjini Arusha ambako ulitarajiwa kupanda ndege nyingine kuendelea na safari.

Waandishi wa habari walipofika katika Uwanja wa Ndege wa Wasso hawakuruhusiwa kuusogelea ujumbe huo kutokana na kile kilichodaiwa kuwa, watu hao walikuwa katika "safari binafsi".Sifa Maanya Kabila ambaye ni mmoja wa wake watatu wa aliyekuwa Rais wa DRC, Hayati Laurent Kabila amekuwa nadra kuonekana hadharani tangu mumewe alipofariki dunia na mtoto wake kuchukua madaraka hayo, hajawahi kuzungumza hadharani wala mbele ya vyombo vya habari.Taarifa za maofisa wa Uhamiaji waliopo Samunge zinabainisha kuwa zaidi ya wageni 500, wengi wao wakiwa raia wa Kenya, wameshafika kijijini hapo kunywa dawa.
Endelea kusoma habari hii.................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits