Tuesday, April 26, 2011

Best Blogger Tips
Liyumba kutoka gerezani?

Via Tanzania Daima

WAKATI Rais Jakaya Kikwete akitoa msahama kwa wafungwa 3,060 katika kuadhimisha miaka 47 ya Muungano, aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba, anatajwa kuwa miongoni mwa walionufaika na msamaha huo.

Habari ambazo Tanzania Daima Jumatano imezipata kutoka kwa watu wa karibu na Liyumba zinapasha kuwa msahama huo unaweza kumnufaisha yeye na wenzake wanaotumikia kifungo kisichozidi miaka mitano ambao hadi jana walikuwa wametumikia robo ya vifungo vyao.

Liyumba alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela baada ya kupatikana na hatia katika shtaka la kutumia madaraka vibaya wakati akiwa mtumishi wa umma.

Kundi lingine litakalofaidika na msamaha huu ni la wafungwa wagonjwa wa ukimwi, kifua kikuu na saratani na ambao wanaelekea kuwa katika siku za mwisho za maisha yao.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha, amesema Rais Kikwete amewasamehe wafungwa wenye ukimwi, kifua kikuu na saratani.
Endelea kusoma habari hii.....................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits