Friday, April 22, 2011

Best Blogger Tips
IJUMAA KUU: Maaskofu wahofia hatima ya nchi

Via Mwananchi

MAASKOFU wa madhehebu mbalimbali ya Kikristo Tanzania, jana waliitumia Ibada ya Ijumaa Kuu ambayo ni ya kukumbuka mateso ya Yesu Kristo, wakielezea wasiwasi wao juu ya hatima ya nchi kutokana na kugubikwa na vitendo vya rushwa na suala zima la utoaji wa haki kwa wananchi.
Waliwataka waumini wa Kikristo na Watanzania kwa ujumla kuitumia Sikukuu ya  Pasaka kurejea vitendo vyema ikiwa ni pamoja na kuheshimiana na kudumisha amani.

Waliozungumza jana ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana nchini, Dk Valentino Mokiwa, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Yuda Thadeus Ruwa’ichi, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Makanisa ya Pentekoste Tanzania (PCT), Askofu David Mwasota, Askofu wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Nestory Timaywa na Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Eusebius Nzigirwa.

Askofu Ruwa’ichi alilia na haki

Kwa upande wake, Ruwa’ichi ambaye ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, alisisitiza umuhimu wa Serikali na dola kutoa haki kwa umma akisema: “Siyo lazima kelele ya wengi inaporindima ndiyo haki inatendeka.”

Akihubiri kwenye ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Epifania, Parokia ya Bugando, Askofu Ruwa’ichi alisema kila mmoja anawajibika kusimamia ukweli ili kuungana na Kristo katika kutenda haki.

Alisema watendaji wa Serikali wanapaswa kujihoji ni kwa kiasi gani wanatimiza mapenzi ya Mungu katika kuwatendea wenzao haki.
Endelea kusoma habari hii......................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits