Saturday, October 15, 2011

Man United yalazimisha sare na Liverpool

Best Blogger Tips
Steven Gerrard akishangilia bao na wenzake
Javier Hernandez aliisawazishia Manchester United zikiwa zimesalia dakika tisa kabla mchezo haujamalizika na kuisaidia timu yake kuambulia angalao pointi moja katika pambano kali dhidi ya Liverpool.

Mshambuliaji huyo anayechezea pia timu ya taifa ya Mexico, aliingizwa mchezaji wa akiba kipindi cha pili, alitumia akili ya haraka baada ya mpira uliochongwa na Danny Welbeck na kufanikiwa kuisawazishia kwa kichwa timu yake ya Manchester United na kuinyima ushindi Liverpool kutokana na bao lililofungwa awali na Steven Gerrard.

Nahodha huyo wa Liverpool alifunga bao katika dakika ya 68 kwa aina ya mikwaju anayofunga sana ya adhabu ndogo na mpira ukaingia langoni na kumuacha mlinda mlango wa Manchester United David De Gea asijue la kufanya.

Jordan Henderson alikosa nafasi nzuri mbili za kuipatia ushindi Liverpool katika dakika za nyongeza kabla mpira haujamalizika, lakini walinzi wa Manchester United walikaa imara na kuokoa hatari zote na hasa mlinda mlango David De Gea.

Kwa matokeo hayo Liverpool wamefikisha pointi 14 wakijikita nafasi ya tano ya msimamo wa ligi ya soka ya England.
Chanzo: BBC

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits