Thursday, October 6, 2011

Steve Jobs wa Apple afariki dunia

Best Blogger Tips
Steve Jobs
Steve Jobs, mwanzilishi msaidizi na aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa kampuni kubwa ya kimarekani ya Apple, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 56. 

Apple imesema "uhodari wake, hisia zake na uwezo wake ulikuwa chanzo cha ubunifu usiohesabika uliostawisha na kuimarisha maisha yetu sote.

Joba alitangaza kuugua saratani ya kongosho mwaka 2004.

Rais wa Marekani Barack Obama alisema kutokana na kifo chake, dunia "imempoteza mtu mwenye upeo"
Bw Obama alisema, " Steve alikuwa miongoni mwa wabunifu muhimu Marekani- mwenye ujasiri wa kutosha wa kufikiri tofauti, shujaa wa kutosha wa kuamini anaweza kubadili dunia, na mwenye kipaji cha kutosha cha kuweza kufanya hivyo.

Taarifa kutoka kwenye familia ya Bw Job imesema walikuwa naye alipofariki dunia kwa amani siku ya Jumatano.

"Katika maisha yake ya kikazi, Steve alijulikana mwenye upeo; katika maisha yake ya binafsi, aliipenda familia yake," walisema, wakiomba faragha na kuwashukuru wale "waliomwombea" katika mwaka wake wa mwisho.

Tim Cook, aliyerithi nafasi yake katika kampuni ya Apple baada ya Bw Job kuachia madaraka mwezi Agosti, amesema aliyemtangulia aliacha "kampuni ambayo yeye pekee ndiye angeweza kuijenga, na nafsi yake maisha itakuwa msingi wa Apple".

Bendera zimeshushwa nusu mlingoti nje ya makao makuu ya Apple huko Cupertino, California, huku mashabiki wa kampuni hiyo wakiacha rambirambi nje ya maduka ya Apple duniani kote.

Cory Moll, mfanyakazi wa Apple wa San Fransisco alisema, "Alichotufanyia ni kama utamaduni, inauma kwa namna ya kipekee kwa kila mtu".
Chanzo: BBC

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits