Sunday, October 2, 2011

Shoga 'Anti Suzy' afichua siri nzito

Best Blogger Tips
SHOGA maarufu jijini Dar es Salaam, Ibrahim Mohamed ‘Anti Suzy’ (25) ameibuka na kutoa siri nzito kuhusu mambo yanayofanywa na mashoga kwa kushirikiana na baadhi ya vigogo
nchini kuwaharibu watoto wadogo wa kiume.

Ametoa tahadhari huku akidai kuwa kama Serikali kwa kushirikiana na watu wengine
haitachukua hatua, kizazi cha kiume cha Watanzania siku zijazo kitapotea katika dunia hii kutokana na ukweli kwamba wimbi la uwepo wa mashoga linazidi kuongezeka kwa kasi.

Anti Suzy ambaye ni mkazi wa Jangwani, pia amejitangaza kuwa ni muathirika anayeishi na Virusi vya Ukimwi kwa zaidi ya miaka 10 sasa na akasema mashoga wengi wameshaambukizwa virusi vya Ukimwi kama yeye na wanaishi kwa matumaini, hivyo kwa kuwa nao ni binadamu, wasingependa kuona watoto wadogo wa kiume wakiharibiwa kama walivyofanyiwa wao.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hizi katika ofisi za gazeti hili zilizopo Mtaa wa Samora, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Anti Suzy alisema hivi sasa wanaume wenye fedha akiwataja kwa jina maarufu la ‘mapedejee’ wanatumia fedha zao kuharibu watoto wadogo huku wengi wao wakijijua kuwa ni waathirika wa Ukimwi.

“Najua kuwa na Ukimwi si mwisho wa maisha lakini si vizuri mtu ukijijua kuwa umeathirika,
ukamwambukiza mwenzako kwa makusudi, kwa kweli sasa hivi hali ni mbaya, wanaume wenye pesa ‘mapedejee’ wanapenda sana watoto wadogo wa kiume,” alisema na kuongeza:

“Wazazi wawe macho sana, sasa hivi mashoga wa rika langu ukienda ukumbi wa starehe au baa, wakijua wewe ni shoga, anakutafuta mtu anakuomba simu ili umtafutie mtoto
mdogo kwa gharama yoyote.

“Mashoga watu wazima hivi sasa hawana soko, wanasakwa watoto wadogo walioko mitaani na hata shuleni,kama Mwalimu hana utu anaweza hata kuuza mtoto wako kwa sababu ya fedha, mtu yuko radhi kukupa pesa yoyote umtafutie mtoto mdogo wa kiume.

“Wanawapenda pia watoto wa kiume wanaochipukia kwenye ushoga ambao siku hizi ndiyo wapo kibao (wengi), watoto wanaharibika sana, wanaowatafuta wanapewa mpaka laki mbili hata zaidi kwa mtoto mmoja”.

Huku akiwataja kwa majina (yanahifadhiwa), Anti Suzy alisema mapedejee hao wana fedha nyingi hivyo wana ushawishi mkubwa, lakini alitoa angalizo kuwa si watu wote wanaoitwa pedejee wana mchezo huo, ingawa alikiri kuwa wengi wao hujitangaza kwa jina hilo wanapotaka kutafutiwa watoto au mashoga wapya kutoka nje ya mkoa kwa wanaoishi Dar es Salaam.

Akizungumzia ongezeko hilo sambamba na maambukizi ya Ukimwi, Anti Suzy aliyezaliwa
Bugando mkoa Mwanza mwaka 1986 akiwa kitinda mimba kwenye familia yao ya watoto watano, alisema hivi sasa mashoga wengi wameambukizwa ugonjwa huo na wengi wao wanafanya biashara ya kujiuza hivyo wanaendelea kuambukiza watu wengine.

Alisema mwanaume akimkuta shoga baa au katika ukumbi wa starehe kwenye Casino, na pembeni ikiwa kuna mwanamke anayejiuza, humchukua shoga jambo linalofanya
kuendelea kuathirika na kuharibiwa vibaya viungo vyao vya siri.

Alidai yeye alizaliwa akiwa na homoni nyingi za kike na wazazi wake walihangaika hospitali bila mafanikio na alipofika darasa la tatu alianza mchezo huo na mfanyabiashara wa kiarabu (jina tunalo) aliyekuwa akifanya kazi za ndani nyumbani kwake akitoka shule ili apate
fedha za mahitaji ya shule, ikiwemo sare.

Anti Suzy alidai mfanyabiashara  huyo alimtorosha kutoka nyumbani kwao Mwanza na kumpeleka Zanzibar ambako alikaa naye nyumba ya wageni (jina tunalo) kwa zaidi ya mwezi mmoja usiku na mchana akimwingilia jambo alilokuja kubaini baadaye kuwa ameharibu maumbile yake ya kiume.

Alisema pamoja na kuwa na wanaume wengine, alihisi ndiye aliyemuambukiza Ukimwi. “Siwezi kusema ni nani kaniambukiza Ukimwi lakini nahisi ni yule mwarabu, maana mashoga wengi nawafahamu wenye Ukimwi amewachezea sana yeye na pia ameharibu watoto wengi sana, sijui hivi
sasa yuko wapi lakini kweli ameharibu watoto sana na kama yupo hai basi huenda anaendelea kuwaharibu,” alibainisha Anti Suzy.

Siri nyingine aliyoitoboa Anti Suzy alidai, akiwa Dar es Salaam alifanya biashara ya kujiuza na kutembea na waume za watu wakiwemo vigogo nchini wanaopenda kutembea na mashoga kuliko wanawake na alikuwa na uwezo wa kutembea na wanaume watano hadi sita kwa siku wakati mwingine bila kinga, kutegemea na uwezo na matakwa ya wanaume hao na mara nyingine aliwalisha
dawa za kulevya na kuwaibia.

“Kweli nilikuwa naiba sana, kuna jamaa nilimlisha dawa, nikaiba na kugeuza mkono wa simu ya chumbani, simu zikapigwa hazipatikani, wakaja kabla sijatoka, wakamkuta jamaa amelala anakoroma mimi nimeshika baadhi ya vitu na pesa, jamani nilipigwaaa! nilipigwaaa! Lakini sikujali maana aibu ilikuwa kwake, ameshachukua malaya (shoga) watu walimjalia mpaka waandishi wa habari walimpiga picha,” alisema.

Aliwataka wanawake wafuatilie mienendo ya waume zao kwa kuwa japo baadhi yao wamejitangaza kuwa na Ukimwi, lakini wanaume wamekuwa wakiwataka na wengine wanawakimbia wake zao na kuwalazimisha mashoga wawalelee watoto wao kama alivyoletewa yeye mtoto wa mwaka mmoja na nusu na mwanaume aliyekuwa akiishi naye kama mume wake ingawa sheria za nchi haziruhusu.
Source: HabariLeo

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits