Friday, October 14, 2011

Matatizo kwa wateja wa Blackberry

Best Blogger Tips
Simu ya Blackberry
Mwanzilishi wa kampuni ya Blackberry Mike Lazaridis amesema huduma zake zitarejea kama kawaida baada ya kukumbwa na matatizo makubwa kwa kipindi cha siku tatu duniani kote.

Mamillioni ya wateja duniani kote walikuta mawasiliano yao ya ujumbe mfupi na barua pepe yakikatizwa nawengi wao walielezea hasira zao kupitia mtandao wa Twitter.

Katika ujumbe wake kwa njia ya video kwenye tovuti ya kampuni hiyo, Bw Lazaridis hakutangaza tarehe yoyote kuhusu ni lini huduma kamili zitarudishwa.

Pia alionya kwamba huenda kukazuka matatizo zaidi baadae.

"Hivi sasa tunafikia viwango vya kawaida katika Ulaya, Mashariki ya Kati, India na Afrika" alisema ,ingawa huenda kukazuka "matatizo" wakati kampuni inaendelea kutanzua malimbikizo ya ujumbe mfupi na barua pepe.

Wakuu wa shirika la RIM ambalo ndilo linalomiliki Blackberry limekua likijibu kwa haraka zaidi manun'guniko ya wateja baada ya malalamiko kwamba hawakuwa na mawasiliano mazuri baada ya kujitokeza kwa matatizo haya.

"Tunajua tumewavunja moyo wateja wetu wengi. Mulitraji mengi kutoka kwetu.Nataraji mengi kutoka kwetu "alisema.

Wateja walianza kuarifu kupoteza huduma kuanzia Octoba 10 na matatizo yakaanza kusambaa duniani kote.

Kampuni ya Blackberry ina hamu kubwa kutaka ionekane inalitatua tatizo hili kwa haraka baada ya matatizo ya mapema wiki hii ambapo ilisema huduma zilirejea kama kawaida kauli iliyopingwa vikali na wateja walioghadhibika.
Chanzo: BBC

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits