Monday, October 10, 2011

Pires wa Cape Verde ashinda Mo Ibrahim

Best Blogger Tips
Bw Pedro Veroan Pires wa Cape Verde
Aliyekuwa rais wa Cape Verde Pedro Verona Pires ametunukiwa dola za kimarekani milioni tano inayotolewa na wakfu wa Mo Ibrahim kwa ajili ya utawala bora barani Afrika.

Kamati inayoshughulikia zawadi hiyo ilisema Bw Pires, aliyeachia madaraka mwezi Agosti, amesaidia kuifanya nchi hiyo kuwa " yenye demokrasia, utulivu na kustawi zaidi".

Tuzo hiyo intakaiwa kutolewa kila mwaka kwa kiongozi anayechaguliwa kidemokrasia na kuondoka madarakani kwa hiari.

Hapajakuwa na mshindi kwa miaka miwili iliyopita.

Kamati hiyo ilisema hakukuwa na mgombea anayestahili.

Tuzo hiyo ya dola za kimarekani milioni tano, inayotolewa kwa zaidi ya miaka 10, ni zawadi yenye thamani kubwa duniani inayotolewa kwa mtu binafsi.

Washindi wa awali ni aliyekuwa rais wa Botswana Festus Mogae na wa Msumbiji Joaquim Chissano.
Chanzo: BBC

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits