Wednesday, July 18, 2012

Dunia yaadhimisha miaka 94 ya Mandela

Best Blogger Tips
 Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini Nelson Mandela leo anatimiza miaka 94 tangu alipozaliwa.

Siku ya kuzaliwa kwake pia inaadhimishwa na Umoja wa Mataifa kutokana na mchango wake katika kuikomboa Afrika Kusini dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi.

Na nchini Afrika Kusini kwenyewe Nelson Mandela, ataadhimisha siku hii na familia yake na Marafiki huku shughuli mbalimbali zikiandaliwa nchini humo kama katika kusherehekea siku hii.

Mwandishi wa BBC wa Afrika Kusini, Omar Murtasa, amesema kuwa Mzee Mandela anaheshimiwa na watu wengi nchini humo, wakitambua juhudi zake za kupigania Uhuru wa Taifa hilo lilolokuwa likiongozwa kirasmi na Ubaguzi wa rangi.

Ripoti zinasema raia wa nchi hiyo hii leo watajitolea kufanya kazi ya kuwasaidia wasiojiweza kwa muda wa dakika sitini na saba kama njia moja ya kuadhimisha siku hii.

Mandela aliachikiliwa huru kutoka gerezani akiwa na umri wa miaka 67.

Mandela alichaguliwa kuwa rais wa Afrika Kusini mwaka wa 1994.
Source: BBC

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits