Friday, July 20, 2012

Mauwaji Colorado

Best Blogger Tips
Mauwaji ya kutisha yametokea katika mji wa Aurora, ambao uko katika jiji la Denver kwenye jimbo la Colorado. Watu 12 wamefariki na wengine 50 wamejeruhiwa katika tukio hilo.

 Muuwaji aliingia katika ukumbi wa sinema (Movie Theater) na kuanza kupiga watu risasi wakati sinema ya Batman inayoitwa “The Dark Knight Rises" ikionyeshwa.

Watu walioshuhudia tukio hilo wanasema mwanzo walifikili wanachoona na kusikia ni sinema, lakini ukweli ni kwamba haikuwa hivyo, muuwaji aliingia kwenye ukumbi huo akitumia mlango wa tahadhali (Emergency exit door) dakika 30 baada ya sinema hiyo kuaanza.

Muuwaji ametambuliwa kwa jina la James Holmes, ana miaka 24, mkazi wa Aurora. Mama yake anaishi San Diego katika jimbo la California.  Alikamatwa kwenye eneo la kupaki magari la ukumbi huo wa sinema.

Rais Barack Obama na mkewe Michele wameelezea masikitiko yao kufuatia mauawaji hayo. Obama alisema kuwa serikali itafanya kila juhudi kuwasaidia watu wa eneo la tukio, la Aurora wakati huu mgumu.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits