Saturday, July 7, 2012

Thabeet asaini miaka miwili Thunder

Best Blogger Tips
 NYOTA wa kimataifa wa mchezo wa kikapu, Hasheem Thabeet wa Tanzania, ambaye ameshindwa kung'ara kwenye Ligi ya NBA tangu aliposhika nafasi ya pili kwenye mashindano ya vyuo mwaka 2009, amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea timu ya Oklahoma City Thunder, limeripoti gazeti la Daily Oklahoman.

Thabeet alitasaini rasmi mkataba huo mpya Julai 11 mwaka huu.Makubaliano ya mkataba huo hayajawekwa wazi, lakini taarifa zinasema kuwa ni mkataba wa kudumu wa misimu yote miwili.
Kwa mujibu wa Oklahoman, Thabeet atalipwa mshahara  wa dola 880,000 (Sh1.3 Bilioni) katika mwaka wake wa kwanza wa mkataba.

Gazeti hilo limeeleza kwamba, mshahara huyo ni mdogo zaidi kulipwa kwenye ligi.Thabeet mwenye urefu wa futi 7.3, anajiunga na timu hiyo mpya, ikiwa ni ya nne kwake katika misimu minne ya kucheza tangu mwaka 2009.

James Harden, Tyreke Evans, Stephen Curry, Jrue Holiday, Brandon Jennings na Ricky Rubio ni miongoni mwa wachezaji waliosajiliwa toka kwenye mashindano ya vyuo baada ya Thabeet mwaka 2009.Akiwa amecheza michezo 135 ya Ligi Kuu ya Kipapu Marekani (NBA), Thabeet  ana wastani wa pointi 2.2 ya kucheza mipira inayorudi na pointi 0.9 ya kuzuia.

Wastani huo ni sawa pointi 1.8 na 2.1 kwa mipira inayorudi katika mechi 20, lakini kwa zile tano ya mwisho akiwa na timu ya Houston, na michezo 15 akiwa na timu ya Portland.
Chanzo: Mwananchi

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits