Monday, February 22, 2010

Best Blogger Tips
Spika Sitta ngoma nzito, atoboa siri ya ujasiri wake

SPIKA wa Bunge Samuel Sitta ametoboa siri ya ujasiri wake akisema inatokana na nguvu za Mungu, ambazo zimekuwa zikimwezesha kutekeleza wajibu wake kwa uhakika, bila kuyumbishwa wala kuogopa kitu chochote.

Katika kujenga kizazi kipya cha viongozi bora wa taifa hili, Spika Sitta alisema vijana wajengewe maadili mema ili kuwaepusha na ufisadi.

Kauli hiyo ya Sitta imetolewa kipindi ambacho baadhi ya watu wamekuwa wakilishambulia Bunge kwamba limewasaliti Watanzania, kutokana na uamuzi wa Spika huyo kufunga mjadala wa kashfa ya Richmond Development (LLC) hivi karibuni.

Wakati makombora hayo yakielekezwa kwenye Bunge analoongoza, jana Spika Sitta alizidi kuonyesha kuwa bado yuko ngangari na kisha kutoboa siri ya ujasiri wake ambayo aliapa kuiendeleza.
Kwa habari zaidi ingia hapa.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits