Tuesday, July 12, 2011

Ludacris ndani ya Serengeti Fiesta 2011

Best Blogger Tips
Via Tanzania Daima

MWANAMUZIKI mahiri wa miondoko ya hip hop ambaye pia ni mwigizaji wa filamu kutoka nchini Marekani, Christopher Brian Bridges ‘Ludacris’ anatarajiwa kutoa shoo ya aina yake kwenye kilele cha tamasha la Serengeti Fiesta 2011, kitakachofanyika viwanja vya Leaders Club, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na kusainiwa na Mkurugenzi wa Maendeleo na Utafiti wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, taratibu zote za kumleta Ludacriss zimekamilika, hivyo Watanzania wakae mkao wa kupata raha wakati wowote kuanzia sasa.

Aidha, aliongeza kuwa, mwanamuziki mwingine wa kimataifa kutoka nje, atatajwa baadaye ambako wote kwa pamoja wanatarajiwa kutumbuiza kwenye tamasha la miaka 10 ya msimu wa dhahabu unaoendelea na Serengeti Fiesta 2011 kwenye viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Julai 30.

Ruge alisema kwamba shamrashamra za kufikia kilele cha miaka 10 ya Serengeti Fiesta 2011 zitakuwa tofauti na zenye msisimko mkubwa, ikilinganishwa na miaka mingine yote iliyowahi kufanyika tamasha hilo, ambalo ni kubwa katika anga ya burudani ndani na nje ya Tanzania ikiwamo Afrika Mashariki kwa ujumla.

Wakati huo huo, Mutahaba ametoa shukurani kwa wakazi wa Mkoa wa Iringa na Mbeya kwa namna walivyojitokeza kwa wingi na kulikubali tamasha hilo ambalo hufanyika mara moja tu kila mwaka.

Wikiendi hii tamasha la Serengeti Fiesta 2011 litakuwa ndani ya mji wa Moshi kwenye uwanja wa Chuo cha Ushirika huku jijini Arusha litafanyika Namatongee.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits