Tuesday, July 12, 2011

Wachezaji wa Eritrea waingia mitini Tanzania

Best Blogger Tips
Via Tanzania

Wachezaji kumi na watatu wa timu ya mpira wa miguu ya Eritrea ya Red Sea mpaka sasa hawajarejea nchini kwao baada ya michuano ya kanda Tanzania, maafisa wamesema.

Baada ya Klabu hiyo ya Red Sea kupoteza ushindi wake katika michuano ya CECAFA ya nusu fainali siku ya Jumamosi, ni nusu tu ya wachezaji wote waliingia kwenye ndege kurejea Eritrea.

Inaripotiwa kuwa hii ni mara ya nne wa wachezaji wa mpira wa miguu kutoka Eritrea wanatoweka.

Vijana wa Eritrea mara kadhaa wanajaribu kukimbia umaskini, seikali ya kibabe na jeshi kujenga taifa.

Katibu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Tanzania Angetile Osiah ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa suala hilo limeripotiwa kwenye vyombo vya sheria kwa ajili ya Uchunguzi.

"Baadhi ya wachezaji waligongana katika tukio la kujaribu kugonga muhuri pasi za kusafiria za wachezaji ambao hawakuwepo wakati wa ukaguzi katika ofisi uhamiaji uwanja wa ndege lakini walipohesabiwa mmoja mmoja iligunduliwa kuwa wachezaji 13," alisema.

Timu ya Tanzania ya Yanga iliwashinda mahasimu wake wa muda mrefu Simba 1-0 katika fainali ya CECAFA Jumapili.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits