Sunday, July 10, 2011

Kakobe, Mtikila wapambana ubalozi wa Marekani

Best Blogger Tips
Via Mwananchi

MCHUNGAJI Christopher Mtikila andaiwa kwamba amevuruga mpango wa kwenda nchini Marekani wa Askofu Zachary Kakobe wa Kanisa la Full Gaspel Bible Fellowship (FGBF).

Mtikila anadaiwa kuuomba Ubalozi wa Marekani nchini kumnyima viza kiongozi huyo mkuu wa FGBF kwa maelezo kwamba ana kesi ya kujibu mahakamani.

Kupitia taasisi ya Liberty International Foundation, Mchungaji Mtikila ameuandikia barua ubalozi wa Marekani nchini, akiutaka usimruhusu Kakobe kwenda nchini humo, kwa kuwa ana kesi ya kujibu.

Akiwa ameorodhesha tuhuma mbalimbali anazoeleza kuwa zinamkabili Askofu Kakobe katika kesi hiyo, Mtikila amesema, mpango wake wa kwenda Marekani, umelenga kuikimbia kesi hiyo.

"Tunaomba Askofu Kakobe asiruhusiwe kwenda Marekani hadi hapo kesi yake Namba 78 ya mwaka 2011 iliyofunguliwa kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania itakapomalizika," alisema Mtikila katika barua hiyo ya Julai 5 mwaka huu.

Mtikila ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa taasisi hiyo ya haki za binadamu, amefafanua kuwa Askofu Kakobe ameshtakiwa na wachungaji watatu wa kanisa lake la FGBF ambao ni Dezedelius Patrick, Angelo Mutasingwa na Benedict Kaduma.

"Anahusishwa na matumizi mabaya ya fedha za kanisa hilo zinazofikia Sh14 bilioni," alisema Mtikila katika barua hiyo na  kuongeza:
“Tunakuandikia kuomba mamlaka zako husika kumnyima Zacharia (Zachary) Kakobe kibali cha kuingia nchini kwako hadi hapo kesi dhidi yake iliyofunguliwa Mahakama Kuu itakapoamuliwa.”

Katika barua hiyo, Mtikila ameueleza ubalozi wa Marekani kuwa Askofu Kakobe anataka kuimbikia kesi hiyo na kuhamia katika mji wa Boston, ambako ataishi na kuendesha taasisi yake inayojulikana kama Bishop Zachariah Kakobe International Ministry.

Mwananchi lilimtafuta Askofu Kakobe juzi na jana ili kufahamu undani wa safari yake ya kwenda nchini Marekani, lakini simu yake ilikuwa ikiita muda wote bila kupata majibu.

Baadaye gazeti hili lilimpata msadizi wake ambaye alisema kwamba askofu huyo asingeweza kuzungumza kutokana na kwamba alikuwa kwenye huduma.
Endelea kusoma habari hii...............

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits