Monday, July 25, 2011

Mwakiteleko taa iliyozimika ghafla - Lowassa

Best Blogger Tips
Via Majira

WAZIRI Mkuu wa zamani, Bw. Edward Lowassa jana alikuwa miongoni mwa mamia ya watu waliofika nyumbani kwa Naibu Mhariri Mtendaji wa New Habari 2006, Marehemu
Danny Mwakiteleko aliyefariki dunia juzi na kusema kuwa waandishi wa habari nchini wamepoteza kiungo mahimu katika tasnia ya habari nchini.

Bw. Lowassa aliyeongozana na mkewe, Regina Lowassa, alisema Bw. Mwakiteleko ni taa yenye mwanga iliyozimika ghafla.

Akizungumza na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nyumbani kwa Marehemu, Tabata Chang'ombe, Dar es Salam jana, Bw. Lowassa alisema Marehemu Mwakiteleko alikuwa mwandishi makini aliyefanya kazi yake kwa ajili ya maslahi ya Taifa.

Alisema wahariri, jamii na Taifa kwa ujumla wamepoteza mwandishi mahili aliyesimama imara kutetea jamii kupitia kalamu yake.

"Mimi binafsi na familia yangu, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo langu la Monduli, tunaipa familia yake pole nyingi. Naomba Mwenyezi Mungu awape nguvu na faraja ya kweli hasa katika kipindi hiki cha majonzi," alisema.

Aliwataka waandishi wa habari nchini kuiga mfano wa uandishi wa marehemu Mwakiteleko.


Kibanda kuwakilisha wahariri

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanazania (TEF), Bw. Absalom Kibanda atawakilisha wahariri wenzake katika msafara wa mazishi ya Marehemu Mwakiteleko mkoani Mbeya.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Katibu wa TEF, Bw. Neville Meena ilisema kuwa katika msafara huo, Bw. Kibanda ataambatana na mwakilishi wa jukwaa hilo kutoka Zanzibar ambaye jina lake halikutajwa.

Bw. Mwakiteleko alifariki dunia saa 10 alfajiri, Jumamosi Julai 23, 2011 kufuatia majeraha aliyoyapata kichwani kwenye ajali ya gari Julai 20, 2011 katika eneo la Tabata TIOT saa nne usiku alipokuwa akirejea kutoka kazini.
Endelea kusoma habari hii.......................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits